Wednesday, October 4, 2017

HATIMAE MWILI WA SHABAAN YOHANA WANTED KUWASILI NCHINI KWA AJILI YA MAZISHI

HATIMAE mwili wa Shabani Yohana Mwanasande, aliyejulikana kwa jina la Shaban Wanted utawasili alfajiri  Jumatatu 9 Oktoba 2017. Shaban Yohana ambae jina lake halisi ni Cloud Yohana Mwanasande alifariki akiwa peke yake chumbani kwake huko Botswana kati ya tarehe 12 na 13 Septemba 2017, jambo lililofanya mwili wake kuwa chini ya vyombo vya usalama kwa muda mrefu. Shukrani kubwa zitolewe kwa jamaii ya Watanzania na wanamuziki wenzake wa huko Botswana kwa kuchangishana na hata kufanya onyesho maalumu la muziki ili kuweza kupta fedha za kufikisha mwili Dar es Salaam. Mwili wa Shabani utapokelewa na wanamuziki wa Tanzania Jumatatu na kisha kupelekwa Muhimbili na kesho yake Jumanne mipango ya kuusafirisha kwenda kwa mazishi Michungwani Muheza itafanyika. Bado michango inahitajika kumalizia safari ya mwisho ya Shabani Wanted. Na atakaeguswa anaombwa kutuma michango kupitia namba 0713274747 na 0763722557 zilizosajiliwa kwa jina la John Kitime.
Shabani Yohana atakumbukwa kwa nyimbo zake alizorekodi kati ya mwaka 1988 hadi 1995 akiwa katika bendi za Tancut Almasi Orchestra, Vijana Jazz Band, na Ngorongoro Heroes. Baadhi ya nyimbo ambazo alipiga gitaa la solo na  bado ni maarufu ni;
Nimemkaribisha Nyoka - Tancut Almasi Orch
Masafa Marefu -Tancut Almasi Orch
Azza- Vijana Jazz Band
Penzi Haligawanyiki -Vijana Jazz Band
Thereza -Vijana Jazz Band
Kamwembwe - Ngorongoro Heroes
Naachia Ngazi - Ngorongoro Heroes
Shime tushirikiane kumzika mpendwa wetu 

No comments: