Saturday, June 17, 2017

MZEE MANYEMA HATUNAE TENA

Mzee Ahmed Manyema hatunae tena, amefariki leo alfajiri katika hospitali ya Mwananyamala. Ni siku chache tu toka kufariki kwa Halila Tongolanga, ambaye walikuwa wote na mzee huyu katika bendi ya Les Mwenge. Mzee Manyema alitunga na kushiriki wimbo wa Chukulubu akiwa  Les Mwenge. Wimbo alioimba akishirikiana na Fredy Siame. Sauti ya Manyema pia ilikuwemo katika nyimbo za Tanga Inter 1978, nyimbo kama Zubeda, Vicky. Halafu alishiriki na Chamwino Bendi alipotunga na kuimba wimbo maarufu wa Waganga wa kienyeji. Mzee Manyema pia alipitia  Jkt Kimbunga na Dar Jazz wakati ikiwa chini ya King Michael Enock,ambapo alitunga wimbo wa Kaka Jirekebishe.Katika miaka ya karibuni alikuwa katika kundi la Sinza Sound, kundi ambalo lilipiga katika hoteli ya Johannesburg Sinza Mori kwa muda mrefu
MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI

No comments: