Tuesday, June 27, 2017

KIPOFU WA MAISHA sehemu ya 1




MSOMAJI HII NI STORY YA KUSISIMUA YA BWANA ERICK MOSHA AMBAE AMEPATA SHIDA SANA KATIKA MAISHA YAKE AKIWA KATIKA SAFARI YA KUTAFUTA  ELIMU MKOANO DODOMA.INALIZA SANA
Ilikua ni asubuhi na mapema ubaridi unaopuliza katika mkoa wa na upepo wa msimu katika mkoa wa Kilimanjaro. Ambapo mama erik na mwanae wakiwa wapo katika hali ya majonzi katika kuagana kwani kijana Erick alikua anaelekea mkoani  Dodoma kwa masomo baada ya kupata nafasi ya kusomea uwalimu kwatika chuo hicho
Mama erik  nenda mwanangu kasome maana elimu ndio kila kitu katika maisha yako (huku akilia )maisha ni magumu sana mwanangu unatakiwa ujitume kadri uwezavyo nitajitahd kuuza ndizi ili usome mwanangu..
Erick nimekuelewa mama yangu nitajituma mama sema najickia vibaya mama kukuacha katika hii hali ya upweke nani atakusaidia hata kukatia majani au kulisha ng`ombe zetu mama yangu?
Mama Erick mwanangu usiniofie mimi huku (akfuta machozi)
Erick sawa mama yangu ila nitakukumbuka sana lakin hatuna budi mama baki salama
Mama alinipa elfu ishirini kama nauli ya mimi kutoka pale kuelekea chuoni udom kwani huko nilipanga kufikia kwa mjomba wangu alieitwa Joshua moshikwani ndie angekua mwenyeji wangu kabla ya kufika chuo. Nakumbuka niliondoka siku ile ndo ilikua mara ya mwisho kumuona mama yangu kipenzi ambae mpaka leo namkumbuka kwani ndie muhimili wangu wa pekee…
Nilibaatika kuzaliwa peke yangu na kulelew na mzazi mmoja Baba yangu aliuwawa wakati bado nikiwa mdogo sana nikiwa na umri wa miaka miwili.siijui raha ya kuwa na baba kama watu wengine. Nililelewa na mama kwa kipindi chote hali ya kuwa hali ya nyumbani ilikua ngumu kwani mama yangu hakuopataga bahati ya kusoma katika uschana wake hivyo alikua mama wa nyumbani na alijitoa sana katika malezi yangu hasa kwenye swala la elimu mama yangu alikuwa akinisih nisome sana ili nikomboe maisha ya nyumbani na kufkia ndoto zangu kwa ujimla.
Nilitoka moja kwa moja nikimuaga mama na kwenda moja kwa moja ambapo nilidandia tatu (daladala)ilionifikisha mpaka  njia panda ya machame ambapo nlisubiri gari znazotoka boma znazoelekea mkoani Dodoma ili kufika kwa mjomba joshua tyr kwa maandalizi ya masomo yangu
Nakumbuka nikiwa njiani nilijinyima kula hali ya kuwa gari nliopanda ilikua mbovu na inasimama mara kwa mara kutokana na ubovu wa safari hiyo.Nilifika mkoani Dodoma majira ya saa 2 usiku nikiwa na njaa sana  moja kwa moja nlielekea katika taxi kadhaa ambazo zilikua karibu na stendi ya mkoa wa Dodoma ambapo niliulizia dereva aitwae Joshua moshakwakua nilikua sina hata simu ya mawasiliano
Kwakua mjomba wangu alikua dereva na alikua maarufu kidogo  maeneo hayo haikua tabu kumpata.Baada ya nusu saa hivi mjomba alifika na alionekana akiwa amelewa akijipiga kifua “jombaa langu limekuja mweshmiwa wa baadae toto pekee la dada yangu” alioneshwa kufurai sana kutokana nay eye na mama yangu kupendana sana . “shkamoo mjomba “ nilimsalimia  lakin alinijibu “shkamoo makelele “ Erick twende zetu kwanza ukapumzike umechoka na safari mimi nina ofa za bia nimeacha huko “ sikumjibu  chochote bali nilionyesha sura ya kukubaliana na wazo lake ambapo nilipanda TAXI yake kuu kuu Nakumbuka sana siku ile katika maisha yangu ni siku ambayo sitaisahau katika maisha yangu  ilikua ni may 16 mwaka 2014 laiti ningejua kama ile siku ingekua  vile basi nisinge hangaika kuitafuta elimu ningalibaki mgombani tu na mama yangu kipenzi.
Tukiwa na mjomba Joshua tunatoka maeneo ya standi ya mkoa Dodoma nikiwa mgeni kidogo nakumbuka tulielekea  magharibi kidogo na stendi mbele kidogo na shule ya sekondari  Dodoma na mbele kidogo ya Bunge la nchi yetu kulikua na mtaa unaitwa makole kama skosei ndipo tulismamishawa na watu wawili ambapo walikua na mwonekano kama abiriA  kwakua nilikua nimekaa siti ya mbele pembeni na dereva  mjomba aliamua kusmamisha gari
“tusiache vichwa pesa ya kufunga hesabu hii mwanangu” aliyasema mjomba  huku akisimamisha gari wale watu walifinguA  mlango na kuingia ndani ya gari walidai kuwa wanataka kuelekea eneo la area d maeneo ya karibu na mlima walitaka kujua bei mjomba aliwambia waandae elfu 5000 maana hata sisi tulikua tukielekea maeneo hayo hayo  bila kusita gari ilirudi tena barabarani na kuanza kuelekea palipotakiwa
Lakini tukiwa njiani Yule abiria wa kiume alipiga simu na kuongea maneno ambayo yalintisha kidogo
“mkuu mzigo tunio lakini viumbe ni viwili andaa mazingira “ kasha akakata simu bila kupata majibu kwa aliempigia au mwitikio  lakini sikujali na nikaendelea kuutazama uzuri wa mkoa wa Dodoma  nakumbuka mjomba aliuliza hali ya mama na watu wengne ambao walikua marafiki pale kijijin alionesha uchangamfu mkubwa pia Nadhani ni kutokana na pombe ilio kichwani.
Tukiwa eneo la ukimya na kama pori eneo ambalo liliitwa area d ghafla tuliona watu watatu wamesimama na kujitandaza  barabarani ghafla abiria tuliokua nao kwenye gari wote wawili wakituambia kwa sauti “simamisha gari mpo chini ya ulinzi” mwanamkwe alimnyooshea njomba silaa ndogo ya moto na Yule mwanaume alitoa panga ambalo aliliweka usawa wa shingo yangu  nilishtuka sana
“hapa asimamishi gari mtu na  leo mmekosea namba  nasema labda tufe woote”  aliyasema hayo maneno mjomba huku akiongeza spidi ya gari straight kuelekea pale wale watu watatu walikua wamesimama  kulizinga gari . nikiwa nimeshikwa na butwaa na nikiusoma mchezo unavokua  nakumbuka wale watu baada ya kuona gari inakuja speed na hakuna dalili ya kusmama waliamua kutoka barabani
“neema uwa huyo mshenzi fyatua ya utosi tumalizee” ilikuz ni sauti ya Yule  mwanaume ghafla gari lilipoteza uelekieo na kuingia porini katika zile purukushani za vitisho. Nikiwa nmapigo ya moyo yanaenda mbio na nikijishkilia vizuri kutokana na kuyumba na mwendo kasi wa gari  niliskia kishindo kikubwa sana katika maskio  ambacho kilipelekea mvurugano ndani ya gari  …..sikumbuki nini kilitokea lakini nlikua nipo chini navuja damu maeneo ya shingo na maumiv makali pia. Nilinitahd kuinuka lakn nilishindwa nilijarib kugeuza kichwa pia niliskia maumivu makali sana . nilijaribu kupaza sauti kuomba msaada lakin niliskia maumiv makali shingoni na pia sauti haikutoka.. nilibaki natokwa na machozi huku nikiwa najihisi kama maskio yangu yameziba………
Mpendwa msomaji usikose sehemu ya pili ya mkasa huu wa kweli wa Erick mosha


No comments: