Monday, May 1, 2017

MSONDO KUTENGENEZA HISTORIA?

HABARI ambazo hazijathibitishwa zimesema kuwa bendi ya Msongo Ngoma Music imechukuliwa tena na Chama cha Wafanyakazi, na itaitwa TUCTA Jazz Band 'Msondo Ngoma'.  Hii itakuwa historia ya mambo mengi, kwanza kurudi kwa uhusiano kati ya bendi hii na vyama vya wafanyakazi. Bendi hii ilianzishwa na chama cha wafanya kazi cha NUTA mwaka 1964 na kuitwa NUTA Jazz Band, na kubadilika kuwa JUWATA Jazz Band baada ya mabadiliko yaliyozaa Jumuiya ya Wafanya kazi Tanzania (JUWATA). Baada ya mabadiliko mengine yaliyoleta chombo kilichoitwa Organization of Tanzania Trade Unions (OTTU), bendi ikabadili jina na kuitwa Ottu Jazz band, kwa muda mfupi kulikuweko mabadiliko mengine yaliyoleta Tanzania Federation of Free Trade Unions (TFTU), na bendi ikachukuliwa na TFTU. Hatimae bendi ikajikuta iko huru ikiendeshwa na wanamuziki wenyewe na ndipo ilipojipa jima la Msondo Ngoma Music Band, na kama inavyosikika inaweza sasa tena ikaitwa TUCTA Jazz Band.hakika itakuwa moja ya bendi ambazo zimewahi kubadili jina mara nyingi kuliko bendi nyingine duniani.

No comments: