Monday, December 15, 2014

BURIANI SHEM IBRAHIM KARENGA

LEO Jumatatu tarehe 15 Desemba 2014, majira ya saa nne asubuhi taarifa zilianza kusambaa kuwa mwamba mwingine wa muziki wa dansi Tanzania umedondoka. Mzee Shem Karenga hatunae tena,kwa vyovyote waliohudhuria dansi alilopiga Ijumaa na Jumamosi iliyopita pale Mwembeyanga watakuwa hawaamini, lakini imekuwa mapenzi ya Mungu, kwamba asubuhi ya leo aliamka hajisikii vizuri na alipelekwa hospitali ya Amana lakini hakukuweza kufanyika kitu Mzee akarudi kwa Muumba wake. Mungu aipokee roho yake. Miezi michache iliyopita tulipata muda mrefu wa kuongea na Mzee Shem Karenga ili kujua alikotokea na mawazo yake kwa sasa mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo;................................. ENDELEA HUKU

No comments: