Saturday, October 11, 2014

ALLY RASHID AZIKWA KEKO

Umati mkubwa wa watu ulijitokeza kumzika Ally Rashid mwanamuziki wa siku nyingi ambaye alifariki jana mchana. Mazishi yalifanyika katika makaburi ya Keko Machungwa  kaburi lake likiwa jirani kabisa na la mwanamuziki mwingine nguli Moshi William. Mazishi ya Mzee Alyy yalifanyika muda wa saa nne asubuhi pia na kuhudhuriwa na wanamuziki wengi wa zamani na hata wa sasa akiwemo Mchizi Mox ambaye alikuwa kimwita marehemu baba yake mdogo.
MUNGU AMLAZE PEMA ALLY RASHID KWA PICHA INGIA HAPA

No comments: