Saturday, January 6, 2018

TASNIA YA MUZIKI 2017 KWA UFUPI

Kuanzia mwaka 2012 nimekuwa nikimaliza mwaka kwa kuandika makala ya mtizamo wangu kuhusu hali ya muziki katika mwaka uliokwisha. Na mwaka 2017 ndio huoo umetokomea, ni vizuri kuangalia yaliyopita ili kujitayarisha na yajayo. Kama ilivyokuwa kwa miaka mingi sasa, anga za muziki wa nchi yetu zilitawaliwa na muziki wa Bongoflava. Muziki ambao kwa asilimia kubwa hutengenezwa studio, hakuna shaka watu wengi  nchini na nchi jirani wametokea kuupenda sana muziki huu. Katika mkutano ulifanyika wiki chache zilizopita, kiongozi mmoja wa mambo ya Hakimiliki kutoka  Kenya alisema asilimia kubwa ya muziki unaopigwa kwenye vyombo vyao vya utangazaji ni wa kutoka Tanzania. Imefika mahali mpaka wasanii wa huko wameanza kudai muziki wa Tanzania upunguzwe ili wao waweze kupata nafasi zaidi katika redio na luninga zao. Inachekesha kuwa kilio kama hichohicho kinasikika kwa wanamuziki wa aina tofauti nchini kuhusiana na ‘kufunikwa’ na Bongofleva. Wasanii wa Bongofleva wameendelea kupata tuzo kutoka kwa taasisi mbalimbali za Kimataifa, na hata wengine kuingia mikataba na kampuni kubwa za kimataifa za usambazaji, na kwa picha hii Bongoflava itaendelea kutawala anga za muziki hata mwaka ujao. Muziki ambao tunaweza kusema chanzo chake ni muziki wa mchiriku wenye asili ya ngoma za Kizaramo, maarufu kama muziki wa singeli nao ulikuja juu sana kwa miezi michache ya mwaka huu, japokuwa ule moto wake unapungua, inawezekana muziki huo unajimaliza wenyewe kutokana na mashahiri yanayotumika katika nyimbo hizo, na hata video zinazo ambatana nazo, lakini hakika muziki huu ni ubunifu unaoweza kuitwa muziki wa asili ya Kitanzania bila shaka yoyote. Hakukuwa na mambo ya kushtua sana katika muziki wa Taarab hali hiyohiyo pia ilionekana katika muziki wa dansi. Bendi kadhaa na vikundi vya taarab vilitangaza kuanzishwa lakini havikuja na kitu kipya cha kuweza kuleta mshtuko katika tasnia, kifupi hakukuwa na jambo lolote chanya la kukumbukwa kutoka upande huo kwa mwaka 2017. Pamoja na kuwa haukuonekana kuwa umeshuka lakini pia hakukuwa na dalili za kupanda kwa muziki wa Enjili, kwenye sanaa usipopanda ujue umeshuka. Muziki wa kwaya ulianza kujitokeza zaidi hasa kwenye kutoa elimu ya mambo mbalimbali ya kijamii na pia kurudia nafasi yake ya zamani ya kusifia viongozi mbalimbali, kazi ambayo kwaya ilikuwa ikifanya toka miaka ya mwanzoni baada ya Uhuru. Kwaya kadhaa ziliweza kutengeneza video ambazo zimekuwa zikionekana kwenye luninga, japo ni wazi hazikutengenezwa kwa ajili ya biashara. Kuna kundi la wanamuziki ambao wao husema huwa hawana nia kabisa ya kusikika kwenye vyombo vya utangazaji vya hapa nchini, wao hutengeneza muziki kwa ajili ya maonyesho ya nje ya nchi. Wanamuziki hawa wameendelea kuwa na safari za kwenda nje kupiga muziki wao katika matamasha ya kimataifa bila kuhangaika kutambulisha kazi zao hapa nchini, sababu kubwa ambayo wamekuwa wakitoa ni urasimu wa taratibu za muziki kusikika katika vyombo vyetu vya utangazaji.  Hivyo badala ya kupoteza muda kupingana na mfumo, wao wameendelea na shughuli za kujitambulisha nje, ni nadra habari zao kuonekana kwenye vyombo vya habari vya nchini japo wanazunguka nchi mbalimbali duniani wakipiga muziki unaotambulika huko kuwa ni wa Kitanzania.  Muziki wa asili  ni kazi ambayo inaonekana ni kwa ajili ya watalii na shughuli maalumu za kiserikali au sherehe za kifamilia. Picha hii inadanganya kwani muziki asili unaendelea nchini mijini na vijijini japo hauonekani kwenye vyombo vya utangazaji, labda pale ambapo ni kiburudisho cha viongozi. Muziki wa asili uko katika makundi mawili, uko muziki ambao unafanywa na wasanii ukiwa ni mchanganyiko wa ngoma mbalimbali ili kuweza kuvutia biashara, na uko muziki asili ambao huchezwa na kuimbwa na wenye kabila lao kwa upenzi wa utamaduni wao. Kwa kuwa hauonekani wala kuzungumziwa sana kwenye vyombo vya utangazaji, unaweza ukadhani haupo au haupendwi lakini hilo si sahihi. Maelfu ya vijana nchi nzima wanacheza na kupiga ngoma za kiasili kwa ufasaha mkubwa.
 Kumekuweko na matamasha kadhaa ya muziki nchini, kama tamasha la Fiesta, Marahaba, Tulia Traditional Dance Festival, Sauti za Busara, Karibu Music Festival na kadhalika, lakini matamasha haya ilikuwa ni nafasi ndogo sana ukilinganisha na idadi ya wanamuziki walioko nchini. Wilaya, mikoa nayo ingeweza kutayarisha matamasha yake ya utamaduni ingekuwa sehemu nzuri sana ya kuendeleza utamaduni, wasanii kubadilishana ujuzi, kuibua vipaji na kuleta burudani kwa wananchi  kwa ujumla. Ufadhili katika shughuli za muziki umekua ukiangalia sana faida za kibiashara, kumekuwa na kampuni chache ikiwa zipo ambazo zimefadhili matamasha kwa nia tu ya kuendeleza muziki. Matamasha mengine yamekuwa yakitegemea ufadhili wa balozi mbalimbali za nje kuwezesha kufanya maonyesho ya muziki wetu. Ni kichekesho kwa kweli. Hata zile kampuni ambazo ni maarufu nje ya Tanzania kwa kuunga mkono shughuli za sanaa, kwa namna ya ajabu zikiwa Tanzania ghafla zinakuwa na msimamo tofauti.
Maeneo ya kufanya shughuli za muziki yamezidi kupungua, mengine yamevunjwa na maeneo kuachwa wazi kama vile eneo lilokuwa DDC Magomeni na Mango Kinondoni, mengine yamekuwa makanisa na kadhalika. Pamoja na kuwa kulikuwa na wimbi la kujenga kumbi ambazo hutangazwa kuwa ni ‘multi purpose’, kumbi hizi haswa zilijengwa kwa ajili ya kufanyia shughuli za harusi, kuna mambo kadhaa ambayo si rafiki kwa muziki katika kumbi hizi, na hata wenye kumbi hukataa kumbi zao kutumika kwa shughuli za muziki hasa wa dansi.
 Katika mwaka 2017  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr Harrison Mwakyembe amekuwa na mikutano mingi na wanamuziki, jambo jema kinachosubiriwa 2018 ni matokeo ya mikutano hii. Ushauri kwa wanamuziki ambao muziki wao unajikongoja, kuna umuhimu wa kutafuta majibu ya kisayansi kwanini hali iko hivyo. Majibu mepesi ya kulaumu vyombo vya habari, serikali na wadau wengine, kamwe hayata saidia katika kuleta mabadiliko.


Thursday, January 4, 2018

WOW Gospel - 2015


Disc 1
01.Perfect People (Kirk Franklin)
02.Give Me(Kirk Franklin.Feat Mali Music.)
03.All I Need is You(Lecrae)
04.Beautiful Day(Jamie Grace)
05.You Are(Erica Campbell)
06.You Love Me (Best of My Love)(Anita Wilson)
07.Worth Fighting For (Brian Courtney Wilson)
08.No Greater Love (Smokie Norful)
09.I Can Only Imagine (Tamela Mann)
10.Live Through It (James Fortune & FIYA)
11.I Believe (Mali Music
12.2nd Win (Kierra "Kiki" Sheard)
13.Here Right Now (Tasha Page-Lockhart)
14.Alright OK (J Moss)
15.I Will Lift Him Up (Fred Hammond)

Disc 2
01.He Turned It (Tye Tribbett)
02.It Pushed Me
03.Dominion (Jason Nelson)
04.Can't Live Without You (William McDowell)
05.Deeper (Marvin Sapp)
06.It's Working (William Murphy)
07.Amazing (Ricky Dillard & New G)
08.God My God (VaShawn Mitchell)
09.For Your Glory (Tasha Cobbs Leonard)
10.Best For Last (Donald Lawrence & Co. Feat. Yolanda Adams)
11.Come As You Are (Donnie McClurkin Feat.Israel Houghton, Marvin Sapp, New Breed Africa.)
12.I Feel Your Spirit (Hezekiah Walker)
13.We Are Victorious (Donnie McClurkin Feat.Tye Tribbett)
14.We've Gotta Put Jesus Back (Kurt Carr Feat. Kurt Carr Singers)
15.Sweeping Through the City (Beverly Crawford)

Click Here To Download

Mandisa - Overcomer - 2013


01.Overcomer
02.Back To You
03.The Distance
04.Face 2 Face
05.Press On
06.What Scars Are For
07.Dear John
08.At All Times
09.Joy Unspeakable
10.Praying For You
11.Where You Begin

Mary Mary - Incredible - 2002


01.Incredible
02.God Bless  Atk
03.He Said
04.In the Morning
05.Ordinary People
06.Trouble Ain't
07.Little Girl
08.This Love
09.I Try
10.Hold On
11.God Has Smiled on Me
12.You Will Know
13.So Close
14.Thank You
15.Give It Up Let It Go

Clique Aqui Para Baixar (Click Here To Download)

J Moss - V4... The Other Side - 2012

Born and raised in Detroit, MI, gospel singer and producer J. Moss is part of a very talented family of gospel musicians, including his father, Bill (of Bill Moss & the Celestials), and his cousin, part of the group the Clark Sisters. Eventually, J. (or James) would start his own group, a duo with brother Bill called the Moss Brothers. Over the next few years, the Moss Brothers would record a pair of albums and tour regionally, but the call of further education lured James away -- but not for very long. It would only be two years in at Michigan State University before J. realized that his true calling was in music, namely putting to work his skills in production and composition. A small-potatoes solo career inked just after returning to Detroit fizzled rather quickly, but it would be his participation in the production trio known as PAJAM that would catapult J. to greater success in his chosen genre. The group, made up of James, Paul Allen, and Walter Kearney, produced and composed a number of gospel hits, using traditional elements of gospel alongside more up-to-date hip-hop and R&B sounds. In 2004, J. Moss, with songs written with his PAJAM partners, decided to give a solo album another shot. The resulting work, The J. Moss Project, was released in 2004 and became a hit. J. decided to keep on working as a solo artist and in 2007 -- after a bit of delay -- released a follow-up entitled V2.... In addition to his already impressive résumé, J. Moss has had a hand in work by other artists such as Patti LaBelle and *NSYNC.


01.God's Got It
02.Imma Do It
04.Strong Enough
05.Good & Bad
06.Good Day (Feat.Karen Clark Sheard & Kierra "KiKi" Sheard)
07.Caught Up in Love
08.Shout
09.You Did (Feat.James Fortune)
10.Holy Is Your Word
11.The Prayers (Feat: Hezekiah Walker, LFP & Dorinda Clark-Cole)
12.The Other Side of Victory
13.Keep Your Head Up
14.Good & Bad [Remix Club Mix]

MTUNZI WA LUNCHTIME MZEE GABRIEL OMOLO AFARIKI DUNIA



Mzee Gabriel Omolo Aginga anayejulikana kwa wapenzi wengi wa muziki wa zamani kwa wimbo wake Lunchtime, alikuwa ni mmoja wa wanamuziki wachache waliotamba Kenya katikamiaka ya 70 ambao walikuwa bado hai. Katika video moja iliyotoka karibuni ilimuonyesha Mzee Gabriel ambae uzeeni alikuwa mkulima akiangalia mifugo yake akiwa katika afya nzuri.
Gabriel Omolo
(Picha kwa hisani)
Gabriel alifariki baada ya kuugua kwa muda mfupi na kufariki katika hospitali ya Busia jana Jumatano usiku. Rafiki yake wa toka utotoni na mwanamuziki mwenzake Charles Makawita ambaye walitoka wote katika kijiji cha Nyabenda Uhoro, kwenye kaunti ya Siaya alisema Gabriel alikuwa na miaka 79 na alifariki kutokana na matatizo ya kushindwa kupumua. Mke wa marehemu Alice Adeya ndiye aliyemtaarifu Charles kuwa mwenzie anaumwa.
Gabriel alizaliwa 1939, alijifunza gitaa akiwa shule ya msingi ya St Peter Claver ambako pia alikuwa anaimba kwenye kwaya ya shule hiyo. Kwenye miaka ya 60 alijiunga na ile bendi maarufu ya Equator Sound Band ambayo wakati huo ilikuwa na miamba akina Peter Tsotsi, Nashil Pichen Kazembe, Daudi Kabaka na Fadhili William. Gabriel ndie aliyepiga gitaa la bezi kwenye wimbo Pole Musa wimbo uliotungwa na Peter Tsotsi. Marehemu Gabriel alipigia pia Eagles Band , Blue Shades na baadae Apollo Komesha Band
Septemba 1974 Gabriel alikuwa Mkenya wa kwanza kupata tuzo ya International Golden Disc kutokana na mauzo ya wimbo wake wa Lunchtime. Kampuni ya Phonogram Records ilihakikisha kuwa single ya wimbo huo iliuza nakala 150,000.Afrika ya Mashariki na Afrika Magharibi.

Remix ya wimbo huo ilifanywa mwaka 2005, ikiwa ni miaka 35 toka ilipoachiwa nyimbo hiyo kwa mara ya kwanza mwaka 1970. Remix ilifanywa na mwanamuziki marehemu Poxi Presha na Paddy makani, Mkongo aliyekuwa akiishi Kenya. Tunamuomba Mungu Amlaze Pema Gabriel Omolo