Wednesday, December 2, 2015

ABOUBAKAR KASONGO MPINDA KUZIKWA LEO KISUTU


MUTOMBO & MPINDA
Marehemu Aboubakar Kasongo Mpinda


MWANAMUZIKI Aboubakar Kasongo Mpinda aliyefariki jana jioni anategemewa kuzikwa leo saa kumi katika makaburi ya Kisutu. Mpinda alifariki jana nyumbani kwake Mwananyamala na mwili wake kwenda kuhifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.
Mungu amlaze Peponi Pema

KASONGO MPINDA CLAYTON HATUNAE TENA


MUTOMBO & MPINDA
Marehemu Mutombo Audax (kushoto), akiwa na marehemu Kasongo Mpinda
HAKIKA siku hii ni ya simanzi, nimetoka makaburi ya Kinondoni ambapo tumemzika mwanamuziki David Musa Gordon wa Safari Trippers, nafika nyumbani taarifa inakuja kuwa mwanamuziki mwingine mkongwe Kasongo Mpinda Clayton amefariki jioni hii nyumbani kwake Mwananyamala na mwili umepelekwa hospitali ya Mwananyamala.
Mungu Amlaze Pema