Monday, November 9, 2015

MWANAMUZIKI MKONGWE CAPT JOHN SIMON AFARIKI DUNIA


IMG_9699
 Capt John Simon
 MWANAMUZIKI mkongwe ambaye kwa siku za karibuni alikuwa kwenye bendi ya Shikamoo Jazz, Capt John Simon, amefariki dunia leo katika hospitali ya Muhimbili. Mzee huyu alikuwa mmoja ya waanzilishi wa NUTA Jazz band, na baadae kadri ya maelezo yake mwenyewe, Mheshimiwa Rashid Kawawa, ndie alimtoa NUTA Jazz na wanamuziki wengine na kwenda kuanzisha JKT Jazz Band, iliyopata umaarufu kama Kimbunga Stereo. 
FIL6
Waimbaji wa NUTA Jazz Band, toka kulia John Simon, Muhidin Gurumo, na kushoto Ally Akida
  Mzee John Simon pia alikuwa mwanzilishi wa Shikamoo Jazz Band, bendi ambayo ameitumikia mpaka siku zake za mwisho. Capt John Simon pia alikuwa makamu mwenyekiti wa CHAMUDATA mwishoni mwa miaka ya 90, akiwa makamu wa John Kitime, na hatimae kuwa mwenyekiti baada ya John kitime kujiuzuru nafasi yake. Taratibu za mazishi zitapatikana baada ya ndugu kukutana. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Tabata Kimanga.

No comments: