NI BAHATI SANA KUWEZA KUPATA VIDEO ZA ENZI BENDI ORCHESTRA MANGELEPA WALIPOKUWA JUKWAANI. NI VIDEO YENYE MAFUNZO MENGI KWA BENDI ZA ZAMA HIZI, JINSI WATU WACHACHE AMBAVYO WALIWEZA KUPOROMOSHA MUZIKI ULIOPANGIKA NA KUTOA SHOW NZURI. NI VIDEO TAMU KWA WAPENZI WA MUZIKI WA DANSI WA ENZI HIZO.....
Tuesday, May 20, 2014
Saturday, May 17, 2014
UNAMKUMBUKA SULTAN SKASSY KASAMBULA?
Kwa wapenzi wa muziki wa dansi wa Afrika ya Mashariki na hasa Tanzania, jina la Skassy au maarufu Sultan Skassy Kasambula si geni hata kidogo, sauti yake ilisikika katika bendi na nyimbo nyingi maarufu. Kwa sasa yuko nairobi na kundi lake la Orchestre Viva Mosukusuku, muangalie na kumsikia katika kazi yake moja kwenye video hii
Thursday, May 8, 2014
DDC MAGOMENI WAVUNJWA RASMI
Kumbi za DDC zilikuwa maarufu sana katika jiji la Dar katika miaka ya 80. Kulikuweko na kumbi za DDC Kariakoo, DDC Magomeni, DDC Keko, zikuwa maarufu kwani wakati huo kulikuwa na uhaba mkubwa wa bia, lakini katika kumbi hizi bia zilikuwa hazikauki, Pia zilikuwa kumbi maarufu kwa madansi na matukio makubwa yakiwemo masumbwi. DDC Magomeni ulikuwa kituo kikubwa cha burudani. Wiki hii ukumbi huo umepigwa nyundo na pamebaki uwanja mtupu ambao kunaelekea kutajengwa kitu. Kuna uwezekano mdogo sana kuwa nafasi hiyo itajengwa tena kwa ajili ya burudani bye bye DDC Magomeni, mengi makubwa ya muziki yalifanyika pale.
Tuesday, April 22, 2014
JIKUMBUSHE ORCHESTRA SAFARI SOUND ENZI ZA MASANTULA LIVE-VIDEO
ORCHESTRA SAFARI SOUND ILIPITIA SURA NYINGI KABLA YA KUONDOKA KATIKA ULIMWENGU WA MUZIKI. KATI YA SURA HIZO NI MASANTULA, DUKUDUKU, NA NDEKULE...VIDEO HII NI KIPINDI CHA MASANTULA
Sunday, April 13, 2014
Monday, April 7, 2014
Sunday, April 6, 2014
PROFESA JUMA BHALO AMEFARIKI DUNIA NA KUZIKWA MOMBASA
Juma Bhalo alizaliwa 1942 huko Shela katika wilaya ya Malindi. Mwaka1954, alijiunga na shule ya msingi ya Sir Ali bin Salim , wakati huohuo familia yake ilihakikisha anahudhuria Madrassa ili kupata elimu ya dini. Bhallo mwenyewe aliwahi kusema hamu yake ya kuimba ilimuanza katika wakati huu na sauti yake kuwa na mvuto kutoka kipindi hiki alipokuwa Madrassa Akiwa na miaka 9 tayari muda wake mwingi ulitumika kusikiliza santuri, na akili yake ilianza kupenda sana muziki. Hakumaliza elimu ya msingi kwa kuwa wazazi wake walishindwa kulipa ada ya shule. Mwaka 1957 alihamia Mombasa na kupata kazi Forodhani, akiwa Mombasa alianza kukutana na kushirikiana na wanamuziki wa Taarab wa Mombasa. Hakuipenda sana kazi ya Forodha hivyo 1959 akahamia Tanga kwa mjomba wake, na hapo akajiunga na kundi maarufu la Taarab wakati ule lililoitwa Young Noverty, hapa alipata ujuzi mkubwa wa muziki wa Taarab.
Alirudi kwao Malindi kwa muda mfupi na hatimae kurudi tena Tanga 1962 na kujiunga na kundi la Young Stars Taarab. Mwaka 1966 alirudi Mombasa na kuanzisha kundi la Bhalo and Party, kundi ambalo amedumu nalo mpaka Mauti yake. Mwaka 2007 baada ya zaidi ya miaka 50 ya kuwemo katika muziki wa Taarab, Juma Bhalo ambaye wapenzi wake walimuita Profesa na hata Mfalme wa Taarab alitangaza kuacha kufanya maonyesho ya wazi ya Taarab, alitangaza hilo siku alipopiga katika harusi ya mwanae. Alistaafu kazi hiyo kwa maneno yafuatayo "Waswahili wasema kiwate kitu kabla hakijakuata. Kwa hivyo kama mulivyo nishuhudiya usiku huu nlivyowatumbuiza ambavyo ni kama kawaida yangu basi leo hii usiku huu kabla hawajaja watu wakasema ahhhhh Bhalo ashazeeka hawezi tena kuimba kwa hivyo najiuzulu ningali bado niko fiti. Kwa hivyo siimbi tena hadharani kikazi. Nawashkuru kwa ushabik wenu na musijali Mungu akiniwezesha Kasseti mpya ntawatoleya".
Alirudi kwao Malindi kwa muda mfupi na hatimae kurudi tena Tanga 1962 na kujiunga na kundi la Young Stars Taarab. Mwaka 1966 alirudi Mombasa na kuanzisha kundi la Bhalo and Party, kundi ambalo amedumu nalo mpaka Mauti yake. Mwaka 2007 baada ya zaidi ya miaka 50 ya kuwemo katika muziki wa Taarab, Juma Bhalo ambaye wapenzi wake walimuita Profesa na hata Mfalme wa Taarab alitangaza kuacha kufanya maonyesho ya wazi ya Taarab, alitangaza hilo siku alipopiga katika harusi ya mwanae. Alistaafu kazi hiyo kwa maneno yafuatayo "Waswahili wasema kiwate kitu kabla hakijakuata. Kwa hivyo kama mulivyo nishuhudiya usiku huu nlivyowatumbuiza ambavyo ni kama kawaida yangu basi leo hii usiku huu kabla hawajaja watu wakasema ahhhhh Bhalo ashazeeka hawezi tena kuimba kwa hivyo najiuzulu ningali bado niko fiti. Kwa hivyo siimbi tena hadharani kikazi. Nawashkuru kwa ushabik wenu na musijali Mungu akiniwezesha Kasseti mpya ntawatoleya".
Taarab yake iliegemea sana muziki wa Kihindi na hivyo kuwa tofauti na taarab nyingine,
MUNGU AMLAZE PEMA PROFESA ,
Kwa wale wanaopenda kusikiliza au kununua nyimbo zake waingie HAPA Angalia video ya mwanae Anwar Juma Bhallo
Subscribe to:
Posts (Atom)




