Friday, August 19, 2016

MAZISHI YA BI SHAKILA , YATAFANYIKA LEO MBAGALA CHARAMBE

Mazishi ya Bi Shakila yatakuwa leo Jumamosi 20 AGOSTI 2016. Mbagala Charambe, saa kumi alasiri Uwanja wa Ninja.
 Namna ya kufika msibani nyumbani kwa marehemu kwa kutumia daladala. Unapanda magari ya Mbagala Rangi Tatu, ukifika mwisho unachukua basi la Nzasa na unashuka Mnara wa Voda hapo unauliza kwa Bi Shakila utaonyeshwa

Sunday, August 7, 2016

LEO TUNATIMIZA MIAKA 12 TOKA KIFO CHA PATRICK BALISDYA


Jina Patrick Balisdya halitakuwa geni kabisa kwa wadau wa blog hii,lazima roho zimeanza kuwadunda kama inavyokuwa kwangu kila nikimkumbuka Blai. Patrick Pama Balisidya alizaliwa Mvumi Dodoma tarehe 18 April 1946. Kabila lake alikuwa Mgogo , kabila ambalo lina wanamuziki wengi maarufu kutokana na muziki kuwa sehemu muhimu ya maisha ya kabila hilo. Mama yake alikuwa anapiga kinanda kanisani na hivyo basi kutokana na asili ya kabila lake na pia kutokana na mama yake, hakika huyu angeweza kujisifu kuwa muziki uko katika damu yake. Mdau mmoja alitutaarifu kuwa Balisidya alikuwa kiongozi wa Bendi ya shuleni kwake Dodoma secondary School. Ambapo kutoka hapo alijiunga na Chuo cha Ufundi , na baada ya kumaliza mafunzo alifanya kazi hiyo kwa muda na 1967 akawa tayari anapiga muziki Dar Es Salaam Jazz B. Kufikia mwaka 1970 Patrick alikuwa ameanzisha kikosi chake mwenyewe Afro70, kikiwa na mtindo wake Afrosa. Alikuwa mbunifu katika muziki wake, na kwa muda mrefu alikwepa sana kuingia katika wimbi la kufuata mapigo ya Kikongo kitu ambacho hata wakati huo bendi nyingi zilikifanya, japokuwa kukutana na Franco wakati alipofanya moja ya ziara zake nchini humu kulimfanya abadili mtindo kwa kipindi kifupi na katika nyimbo moja wapo aliiga kabisa solo la Franco alilolipiga kwenye wimbo wake Georgette. Afro70 iliwakilisha wanamuziki wa Tanzania katika maonyesho ya mtu mweusi Lagos, Nigeria. (FESTAC festival 1977). Vyombo alivyotumia katika maonyesho haya vilimsumbua akili mpaka alipofariki, kwani muda mchache kabla ya Festac, wakati huo serikali ikiwa imeshamtaarifu kuwa ndie atakuwa mwakilishi wa Tanzania, vyombo vyake vyote vilihalibika katika ajali ya gari. Serikali ilikuwa imenunua vyombo vipya kwa ajili ya bendi yake ya Wizara ya Utamaduni wakati huo, ambavyo siku zote Balisdya alisema aliambiwa ni vyake baada ya maonyesho. Aliporudi kutoka Nigeria Kiongozi mwingine wa serikali aliamuliwa arudishe hivyo vyombo virudishwe serikalini na kwa kitendo kile kutangaza kifo cha Afro70. Vyombo hivyo vilitumika kuanzisha bendi ya Asilia Jazz ambayo ilikuwa Bendi ya Wizara ya Utamaduni na Vijana. Balisdya alitumia muda mwingi kujaribu kudai haki yake hiyo ambayo ilimkwepa mpaka mwisho wa maisha. Mwaka 1979, Balisidya alikwenda Sweden na kushirikiana na kikundi cha Archimedes akatoa album nzuri sana iliyoitwa Bado Kidogo. Kuna wakati Patrick alijiunga na Orchestre Safari Sound, (masantula) na kupiga piano katika ule wimbo maarufu, ‘Unambie siri’, Patrick pia alikuwa mpigaji mahiri wa keyboards. Kwa kweli nyimbo za Patrick zilizokuwa juu katika chati ni nyingi. Harusi, Dirishani, Weekend, Tausi, Pesa, Nakupenda kama Lulu, Ni mashaka na mahangaiko, Afrika. Patrick alifariki tarehe 7, Agosti 2004 na kuzikwa 12 Aug katika makaburi ya Buguruni Malapa. Daima tutakukumbuka Patrick Pama Balisidya, Mungu akulaze pema peponi


NI MIAKA 46 TOKA KIFO CHA BAVON MARIE MARIE






Bavon Marie Marie, mdogo wake Franco Luambo,
alizaliwa May 27, 1944 katika jiji la Kinshasa na kupewa jina la Siango Bavon Marie Marie. Alipokuwa mdogo hakuwa mtukutu lakini alikuwa na akili sana, akajulikana sana kwenye eneo alilokulia   wilaya ya Bosobolo. Kadri alivyokuwa akaanza kuishi maisha ya  makeke zaidi kwa kuwa mlevi mzuri wa pombe na msafi aliyechichumbua kisawasawa kama ilivyokuwa desturi ya vijana wa Kinshasa wakati ule. Kama alivyokuwa kaka yake Franco Makiadi naye alikuwa mpiga gitaa mzuri sana. Alipigia bendi kama Cubana Jazz akiwa na mwanamuziki Bumba Massa, akapigia Orchestre Jamel kabla ya kuingia Negro Succes, bendi ambayo ilianzishwa 1960 za Vicky Longomba (Baba wa Awilo Longomba). Vicky aliwahi kuwa mmoja wa wanamuziki wa TP OK Jazz, sasa yeye  pamoja na wenzie Leon’ Bholen’ Bombolo, na mwimbaji mwenzie Hubert ‘Djeskin’Dihunga, mpiga sax Andre Menga, rhythm Jean Dinos, mpiga bezi Alphonse ‘Le Brun’ Epayo, mpiga drum Sammy Kiadaka na mwimbaji mwingine Gaspard ‘Gaspy; Luwowo wakaanzisha hiyo bendi kali kabisa  Negro Succes . Bavon akawa mpiga gitaa wa bendi hii baada ya mwaka 1965, yeye na mwenzie Bholen wakawa viongozi na masupastar wa wakati huo kwa vijana wa Kinshasa. Pamoja na kuwa kaka yake Franco  ndie aliyekuwa akijulikana kama Mwalimu Mkuu wa Rhumba la Kongo yeye pia alikuwa kipenzi  vijana kutokana na upigaji wa solo lake lililokuwa na uchangamfu zaidi .



Tarehe 5 Agost 1970 Bavon Marie alifariki katika ajali ya gari baada ya ugomvi uliotokana na mpenzi wa Bavon aliyeitwa Lucy, ambapo Bavon alimshutumu kaka yake kuwa kalala na mpenzi wake huyo. Ajali hiyo ilisababisha Lucy akatike miguu. Kuna watu wengine wanasema kisa kilikuwa ni ulevi tu wa Bavon ulisababisha bendi yake ishindwe kufanya show nae akawa kakasirika kwa hilo na kuendesha gari kwa fujo na kuishia chini ya uvungu wa roli kwenye njia panda. Pamoja na upigaji wa gitaa Bavon pia alikuwa mtunzi mzuri sana wa mashahiri ambayo yaliwagusa watu. Kwa mfano wimbo wake wa 'Mwana 15 Ans'…Mtoto wa miaka 15, Bavon aliongea kama binti wa miaka 15 ambae ana uchungu kwa kuwa familia yake inamtafutia mchumba japo yeye anataka kwenda shule. Hadithi ambayo wote tutakubali mpaka leo inamaana sana katika jamii za Kiafrika

Wednesday, August 3, 2016

TODAY I WOKE UP WITH THE SONG KWA MJOMBA BY URAFIKI JAZZ BAND


I woke up today with a 1970s Urafiki Jazz Band's tune Kwa Mjomba singing in my brain. The song was composed by Frank Masamba who was a vocalist then but now a saxaphonist and also teaches saxophone. The lyrics of this song  talk about this young guy who visited his uncle and met his beautiful cousin and fell in love with her, but was told he could not marry his cousin but wait for any other girl and someday will fall in love again. The song was very popular during its days, and is still being aired in some radio programs to date. Here are the lyrics;
Nilipokwenda kwa mjomba, Nilikutana na binamu yangu,
Na kwa kweli tulipendana, wazazi wetu walitukatalia tusioane
Eti kwa sababu yeye ni mtoto wa mjomba,
Ndivyo ilivyokuwa vigumu kwetu kufunga ndoa
Nilipokwenda kwa mjomba, Nilikutana na binamu yangu,
Na kwa kweli tulipendana, wazazi wetu walitukatalia tusioane
Eti kwa sababu yeye ni mtoto wa mjomba,
Ndivyo ilivyokuwa vigumu kwetu kufunga ndoa

       Chorus
Wazazi ninansema nasononeka, kwa vile msichana nilimpenda
Basi mwanangu nakuomba usisikitike sana , tuliza roho dunia hii ni pana sana kijana
Wazazi ninansema nasononeka, kwa vile msichana nilimpenda
Utampata wako mwingine pia utampenda, mtoto wa mjomba kweli kuoana si vizuri

Wazazi ninansema nasononeka, kwa vile msichana nilimpenda
Basi mwanangu nakuomba usisikitike sana , tuliza roho dunia hii ni pana sana kijana
Wazazi ninansema nasononeka, kwa vile msichana nilimpenda
Utampata wako mwingine pia utampenda, mtoto wa mjomba kweli kuoana si vizuri

The bands style was 'Mchakachaka' but fondly named 'Chakachua'. The word has changed its meaning now mostly because politicians have made it famous making it mean hoodwinking.  Urafiki Jazz Band was formed in 1970. It was owned by a textile mill known then as  FRIENDSHIP TEXTILE MILL. The company was so named as a sign of friendship between Tanzania and China. It was the Chinese who built the mill.The bands main purpose was to advertise the Khanga and Vitenge products that were being manufactured by the mill. At the time there was stiff competition from other textile mills like Mwatex , Kiltex, Mutex, and so on. The then General Manager of the mill, Mr Joseph Rwegasira (late) dished out 50,000/- which was enough to buy a set of music instruments from Dar es Salaam Music House. The shop is still in business to date. The company management engaged Mr Juma Feruzi Mrisho aka Ngulimba wa Ngulimba a veteran vocalist to come up with a band. Ngulimba took 5 musicians from the band he had just left, African Quilado and they became the core of the new band. He brought in  Michael Vincent Semgumi a lead guitarist, to date one of the best lead guitarists Tanzania has ever come up with, Ayoub Iddi Dhahabu on the bass guitar, Abassi Saidi Nyanga,Tenor Sax, Fida Saidi on Alto Sax. Other musicians were already employees of the company, like Juma Ramadhani Lidenge on the Second Solo guitar, Mohamed Bakari Churchil on rhythm guitar, Ezekiel Mazanda also a  rhythm guitarist, Abassi Lulela another bass guitarist, Hamisi Nguru, Mussa Kitumbo, Cleaver Ulanda all being vocalists, Maarifa Ramadhani on the congas, Juma Saidi on maraccass and Hamisi Mashala playing the drums . That was the firs line up of Urafiki Jazz Band. The band began with its 'Mchakamchaka' style later on changed to 'chakachua' and in its last day in the 80s went on to ‘Pasua’ and lastly ‘Patashika’. Many musicians joined and left this band other famous names of the time include Gideon Banda the saxophonist from  Morogoro Jazz, Thobias Cosmas Chidumule still famous vocalist who has now turned to gospel music, who together with Frank Mahulu joined the group coming from another great group The Western Jazz Band that was sometimes in 1973. Mkali and Hidaya,Trumpet blowers from the nearby town Morogoro accompanied by Ali Saidi, a rythm guitarist from Cuban Marimba, joined the band and in 1975 Mganga Hemedi a rythm guitarist from Atomic jazz band of Tanga joined this great group. Urafiki Jazz Band recorded more than three hundred songs covering subject like love, politics and everyday life in Tanzania at the time. A number of its songs are still being aired and some groups have even recorded their version of the songs. In
1975 the band took part in a Band competition which was held at Mnazi Mmoja Grounds and came third, this gave a ticket to the Band leader Ngulimba to travel with the band that won ( Afro 70 Band) to Lagos for the FESTAC festival held that year.